Thursday, 12 January 2017

NISHAPENDWA, KUPENDA TENA SIWEZI















kupendwa nilishapendwa, kupenda tena siwezi.
Mapendoni nikalindwa, 'sinitukuwe jambazi.
Na kurandwa ninarandwa, na wangu alo mjuzi. 
Nishampata azizi, tena sitaki kupendwa.
Mi si wakupindwapindwa, natangaza waziwazi .
Maudhiko nijetendwa, kwa mitego ya bazazi.
Kwani mtendi katendwa, mida yile chipukizi.
Nimetegwa mteguzi, na nyumbani nikatindwa.
Kiwa kukandwa nakandwa, maungoni kwa henezi.
Mahabani nikafundwa, kwa yake mema malezi.
Ngalikuwa ungashindwa, manake we we huniwezi.
Nishapata wa saizi, ungali wa andwa andwa.
Na usije ukapandwa, na mori wa sisimizi.
Mtimani ukarindwa, na hasira za mkizi.
Ukakuwa umegandwa, na yangu masimulizi.
Hivo kuwa msikizi, phibbiyanni nishapendwa.
Malenga mlezi
Phibbian Muthama
(c)2016

No comments:

Post a Comment