UJANA
Maisha ni neno pana, Maanae sifukui
Mapacha weza fanana, Kwenye kiza huwajui
Hodihodi waungwana, Nivalisheni kikoi
Ya jana mpe kijana, Uzee asitumai
Ya jana ndo ya ujana, Mzee sijisumbui
Hapo maisha hubana, Na kuhisi hupumui
Shida zikafumukana, Mithili utandubui
Ya jana mpe kijana, Uzee asitumai
Starehe za ujana, Mengi hauyang’amui
Hasa upatapo bwana, Hufanya hujitambui
Ila mtapotengana, Maziwa taona tui
Ya jana mpe kijana, Uzee asitumai
Ujana kubwa hazina, Kama mlima sinai
Ukicheza danadana, Hilo kosa la jinai
Mwisho chochote hakuna, Uzee utakudai
Ya jana mpe kijana, Uzee asitumai
Leo ilikua jana, Wakati hauzubai
Tumia vyema ujana, Dhalili nakupa rai
Ujana ulevi bwana, Uzee ni jitmai
Ya jana mpe kijana, Uzee asitumai
Tamati ninafikia, Mbele tena sisogei
Vyema ujana tumia, Afya isikulaghai
Usije ukajutia, Uzee ukisabai
Ya jana mpe kijana , Uzee asitumai
LIMETUNGWA NA NASRI KIONE
0752300012 nasriibrahimu@gmail.com
(FB) TUNGO ZENYE ULIMBO
Hapo maisha hubana, Na kuhisi hupumui
Shida zikafumukana, Mithili utandubui
Ya jana mpe kijana, Uzee asitumai
Starehe za ujana, Mengi hauyang’amui
Hasa upatapo bwana, Hufanya hujitambui
Ila mtapotengana, Maziwa taona tui
Ya jana mpe kijana, Uzee asitumai
Ujana kubwa hazina, Kama mlima sinai
Ukicheza danadana, Hilo kosa la jinai
Mwisho chochote hakuna, Uzee utakudai
Ya jana mpe kijana, Uzee asitumai
Leo ilikua jana, Wakati hauzubai
Tumia vyema ujana, Dhalili nakupa rai
Ujana ulevi bwana, Uzee ni jitmai
Ya jana mpe kijana, Uzee asitumai
Tamati ninafikia, Mbele tena sisogei
Vyema ujana tumia, Afya isikulaghai
Usije ukajutia, Uzee ukisabai
Ya jana mpe kijana , Uzee asitumai
LIMETUNGWA NA NASRI KIONE
0752300012 nasriibrahimu@gmail.com
(FB) TUNGO ZENYE ULIMBO
No comments:
Post a Comment