MAMBA NA KIBOKO
Nimechoka sokomoko, mkulima wa Mnavu
Kila siku chokochoko,ninapofata unyevu
Leo naketi kitako,kuteta na wamabavu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
Mimi langu nung’uniko,ni tabia yenu mbovu
Mwaligeuza tandiko,shamba langu endelevu
Sasa mwaninyima soko,kwa hayo yenu maovu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
Mwafahamika si koko, bali viumbe tulivu
Kajibebea ujiko, maji ndo chenu kitovu
Tulieni huko huko,mkiupata uchovu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
Menikwangua ugoko,nusu niwe mlemavu
Nawaomba badiliko,bado mnaona wivu
Hili ndo lenu anguko,takaloleta kivumvu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
Ngoja nikivute kiko,kusudi nipate nguvu
Niandae mlipuko,wa vyuma vyangu chakavu
Tawafanya rikoriko,nijipatie wagivu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
Wenzangu nipeni heko,mkulima si pumbavu
Bora kusema kuliko,kuonekana mvivu
Kama kwenu ni kicheko,kwangu mimi maumivu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
©2014 Na Innocent Zephania.
Mwaligeuza tandiko,shamba langu endelevu
Sasa mwaninyima soko,kwa hayo yenu maovu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
Mwafahamika si koko, bali viumbe tulivu
Kajibebea ujiko, maji ndo chenu kitovu
Tulieni huko huko,mkiupata uchovu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
Menikwangua ugoko,nusu niwe mlemavu
Nawaomba badiliko,bado mnaona wivu
Hili ndo lenu anguko,takaloleta kivumvu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
Ngoja nikivute kiko,kusudi nipate nguvu
Niandae mlipuko,wa vyuma vyangu chakavu
Tawafanya rikoriko,nijipatie wagivu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
Wenzangu nipeni heko,mkulima si pumbavu
Bora kusema kuliko,kuonekana mvivu
Kama kwenu ni kicheko,kwangu mimi maumivu
Mbona mamba na kiboko,mwaniwinda nchi kavu?
©2014 Na Innocent Zephania.
No comments:
Post a Comment