OA
Oa nakwambia kaka, singoje kunasiwa,Oa yapita miaka, ‘site ngoma kupigiwa,
Oa ‘epuke kumaka, usije kulia ngowa,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa walio na maadili, so sura kuangaliya,
Oa wenye uhiimili, epuka wenye umbeya,
Oa wenye muamali, nyumbani watatuliya,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa hata wa mjini, bora kwa mda kumjuwa
Oa aliye wa kuamini, sumu sije kutiliwa,
Oa kaka kwa makini, sije sema “ningejuwa,”
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa ukiwa kijana, ndoa mapema ku’ngiya,
Oa ulipe dhamana, vyema watoto kuleya,
Oa wajua ujana, ni moshi wa kufukiya,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa wakujitafutiya, nasaha yangu natowa,
Oa uliye dhamiriya, sio mke kuletewa,
Oa tena nakwambiya, sitake wakunadiwa,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa uepuke upweke, na msongo kujitiya,
Oa ukiwa na makeke, kabla uzee kuingiya,
Oa uhuni sitake, sije kufa kwa uthiya,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa upate mwandani, kwa ubani kufukiwa,
Oa kitu cha dhamani, kinda bata na njiwa,
Oa na umweke ndani, waambiwe umeowa,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
©2014 WILLY LUSIGE
"Malenga wa kuvizia"
Oa wenye uhiimili, epuka wenye umbeya,
Oa wenye muamali, nyumbani watatuliya,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa hata wa mjini, bora kwa mda kumjuwa
Oa aliye wa kuamini, sumu sije kutiliwa,
Oa kaka kwa makini, sije sema “ningejuwa,”
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa ukiwa kijana, ndoa mapema ku’ngiya,
Oa ulipe dhamana, vyema watoto kuleya,
Oa wajua ujana, ni moshi wa kufukiya,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa wakujitafutiya, nasaha yangu natowa,
Oa uliye dhamiriya, sio mke kuletewa,
Oa tena nakwambiya, sitake wakunadiwa,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa uepuke upweke, na msongo kujitiya,
Oa ukiwa na makeke, kabla uzee kuingiya,
Oa uhuni sitake, sije kufa kwa uthiya,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
Oa upate mwandani, kwa ubani kufukiwa,
Oa kitu cha dhamani, kinda bata na njiwa,
Oa na umweke ndani, waambiwe umeowa,
Oa uhisi mwenyewe, moyo utakavyopowa.
©2014 WILLY LUSIGE
"Malenga wa kuvizia"
No comments:
Post a Comment