Monday, 23 November 2015

NANI NADHIFU



Msafiri napata safari, neno maana kulitafutia
Kutembea kila mandhari,tanzania hadi India
Ndege hata gari, bila hofu najipandia
machache yanipa tahayari,makubwa napata shangalia
Hakuna katu nadhifu,Mola yeye pekee

Sasa nachambua majibu,niliyopata kule safarini
Nakupeni wangu maswahibu,shuleni na mitaani
Sizidishi nikaja haribu,niliyopata kule mafichoni
kusema kweli thawabu,hujazwa tele thamani
Hakuna katu nadhifu, Mola yeye pekee

Kalamu ikiwa nene,muandiko huwa tafauti
Wanaume waringia wanne,wakikerwa huandika cheti
Wataka shamba wavune,bila kupalilia mti
Kuchezesha na sebene,mafunzo yale karati
Hakuna katu nadhifu, Mola yeye pekee

Waume wengine wajisahau,kurudi nyumbani usiku
Wake zao kuwadharau,michepuko wala kuku
wakirudi wajawa nahau, hawawezi kula daku
Kuwaita paka nyau,kugusana tena marufuku
Hakuna katu nadhifu,Mola yeye pekee

Kasheshe kina mama, wao wametia nukta
Wamesahau kivazi bahama,mjini kitop bukta
Hakuna tena kilema,fesheni kupanda ukutana
Ukipitwa na sinema,mitaani dhahiri utakuta
Hakuna katu Nadhifu, Mola yeye pekee

Jaribu kumuweka ndani, utaona adha yake
Wengine watoka ndoani,kuonjesha jirani zake
Anampenda yule wa zamani,huwezi mfanya aridhike
Talaka ipo mdomoni,huo Wimbo wake.
Hakuna katu nadhifu,Mola yeye pelee

Narudi kwako hadhira,usihukumu mtu mapungufu
Tuombe nasi nusura,yasitupate hayo machafu
Tujilinde na madhara,penzi lisipate Uhalifu
Tuchukizwe na hasira, Ndoa tusije zihalifu.
Hakuna katu Nadhifu,Mola yeye pekee


No comments:

Post a Comment