MASHAIRI YASO VINA!
Mtunzi nimechutama,kusoma yasosomeka.
Imebidi kulalama,na kalamu kuishika.
Niwajuze himahima,niache kusononeka.
Mashairi yaso vina,ladha take hupotea.
Imebidi kulalama,na kalamu kuishika.
Niwajuze himahima,niache kusononeka.
Mashairi yaso vina,ladha take hupotea.
Ladha take hupoteya,mashairi yaso vina.
Msomi huwayawaya,hulisoma akinuna.
Pia huliita baya,hamu fahamu hakuna.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Msomi huwayawaya,hulisoma akinuna.
Pia huliita baya,hamu fahamu hakuna.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Likifwatia urari,vina viwe mufatano.
Vina vikuwe chanjari,shairi lisewe ngano.
Lipangike kwa uzuri,tungo ikawe mfano.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Vina vikuwe chanjari,shairi lisewe ngano.
Lipangike kwa uzuri,tungo ikawe mfano.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Kwa langu hili shairi,mfano nitaangaza.
Msome na mfikiri,muone niloliwaza.
Mwone Halina fahari,lenyewe linajikwaza.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Msome na mfikiri,muone niloliwaza.
Mwone Halina fahari,lenyewe linajikwaza.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Hapa vina siviweki,tofauti ioneni.
Halipendezi machoni,ubeti una kasoro.
Urari haupo on a,linaudhi kilisoma.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Halipendezi machoni,ubeti una kasoro.
Urari haupo on a,linaudhi kilisoma.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Ubeti huo someni,urari haupo ndani.
Ladha haipo wendani,KI NI na tazameni.
Hitilafu mesheheni,Ni To na Ma oneni.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Ladha haipo wendani,KI NI na tazameni.
Hitilafu mesheheni,Ni To na Ma oneni.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Nimewajuza wandani,yaso vina tambueni.
Mkisoma hazarani,yanazua ubishani.
Husumbua kiyaghani,furaha huwa huzuni.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Mkisoma hazarani,yanazua ubishani.
Husumbua kiyaghani,furaha huwa huzuni.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Utunzi wa.
Sauti ya babu.
Mstahiki Zack.
Sauti ya babu.
Mstahiki Zack.
No comments:
Post a Comment