Monday, 23 November 2015

NANI NADHIFU



Msafiri napata safari, neno maana kulitafutia
Kutembea kila mandhari,tanzania hadi India
Ndege hata gari, bila hofu najipandia
machache yanipa tahayari,makubwa napata shangalia
Hakuna katu nadhifu,Mola yeye pekee

Sasa nachambua majibu,niliyopata kule safarini
Nakupeni wangu maswahibu,shuleni na mitaani
Sizidishi nikaja haribu,niliyopata kule mafichoni
kusema kweli thawabu,hujazwa tele thamani
Hakuna katu nadhifu, Mola yeye pekee

Kalamu ikiwa nene,muandiko huwa tafauti
Wanaume waringia wanne,wakikerwa huandika cheti
Wataka shamba wavune,bila kupalilia mti
Kuchezesha na sebene,mafunzo yale karati
Hakuna katu nadhifu, Mola yeye pekee

Waume wengine wajisahau,kurudi nyumbani usiku
Wake zao kuwadharau,michepuko wala kuku
wakirudi wajawa nahau, hawawezi kula daku
Kuwaita paka nyau,kugusana tena marufuku
Hakuna katu nadhifu,Mola yeye pekee

Kasheshe kina mama, wao wametia nukta
Wamesahau kivazi bahama,mjini kitop bukta
Hakuna tena kilema,fesheni kupanda ukutana
Ukipitwa na sinema,mitaani dhahiri utakuta
Hakuna katu Nadhifu, Mola yeye pekee

Jaribu kumuweka ndani, utaona adha yake
Wengine watoka ndoani,kuonjesha jirani zake
Anampenda yule wa zamani,huwezi mfanya aridhike
Talaka ipo mdomoni,huo Wimbo wake.
Hakuna katu nadhifu,Mola yeye pelee

Narudi kwako hadhira,usihukumu mtu mapungufu
Tuombe nasi nusura,yasitupate hayo machafu
Tujilinde na madhara,penzi lisipate Uhalifu
Tuchukizwe na hasira, Ndoa tusije zihalifu.
Hakuna katu Nadhifu,Mola yeye pekee


Sunday, 22 November 2015

MASHAIRI YASO VINA!


Mtunzi nimechutama,kusoma yasosomeka.
Imebidi kulalama,na kalamu kuishika.
Niwajuze himahima,niache kusononeka.
Mashairi yaso vina,ladha take hupotea.
Ladha take hupoteya,mashairi yaso vina.
Msomi huwayawaya,hulisoma akinuna.
Pia huliita baya,hamu fahamu hakuna.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Likifwatia urari,vina viwe mufatano.
Vina vikuwe chanjari,shairi lisewe ngano.
Lipangike kwa uzuri,tungo ikawe mfano.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Kwa langu hili shairi,mfano nitaangaza.
Msome na mfikiri,muone niloliwaza.
Mwone Halina fahari,lenyewe linajikwaza.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Hapa vina siviweki,tofauti ioneni.
Halipendezi machoni,ubeti una kasoro.
Urari haupo on a,linaudhi kilisoma.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Ubeti huo someni,urari haupo ndani.
Ladha haipo wendani,KI NI na tazameni.
Hitilafu mesheheni,Ni To na Ma oneni.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Nimewajuza wandani,yaso vina tambueni.
Mkisoma hazarani,yanazua ubishani.
Husumbua kiyaghani,furaha huwa huzuni.
Mashairi yaso vina,ladha yake hupotea.
Utunzi wa.
Sauti ya babu.
Mstahiki Zack.